Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2024

Elimu kuhusu mikataba ya ajira

  1. NI SHERIA GANI INAYOSIMAMIA MIKATABA AJIRA TANZANIA? Kwa ujumla Sheria ya Mikataba inasimamia aina zote za mikataba Tanzania. Lakini kwa mikataba mahususi kuna sheria mahususi inayosimamia mikataba hiyo. Kwa mfano Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi inaelezea mikataba ya ajira. Kwa maana hiyo ni sawa kusema Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi  ya mwaka 2004 pamoja na Sheria ya Mikataba zote zinasimamia mikataba ya ajira.   KUNA AINA NGAPI ZA MIKATABA? Kuna aina kuu tatu (3) za mikataba ambazo unaweza kuajiriwa nayo, nazo ni:  •    Mkataba kwa kipindi cha muda usiotajwa: Kama jina linavyojieleza, kwa aina hii ya mkataba kipindi cha ajira hakiainishwi. Mara nyingine huitwa mkataba wa kudumu.  •    Mkataba kwa kipindi cha muda kilichotajwa: Hii ni aina ya mkataba ambao umetaja kipindi cha muda. Chini ya mkataba huu kama kipindi kilichotajwa kikimalizika basi mkataba utakua umefikia mwisho. Mkataba wa kipindi cha muda uliotajwa u...

Mchezaji aliyesemekana kuumia AFCON aonekana Spain akicheza

 Dakika ya 73 ya mchezo wa kombe la mfalme maarufu kwa jina la Copa Del Rey nchini Hispania kati ya Osasuna na Real Sociedad January 17, Kocha wa Real sociedad alimnyanyua Umar Sadiq kutoka benchi na kumuingiza ili kuchukua nafasi ya Andre Silva. Tukio hilo la staa huyo wa Nigeria liliwashangaza wengi uwanjani kwani mchezaji huyo alikua kwenye kikosi cha timu ya taifa kule Abidjan nchini Ivory Coast akijiandaa kucheza kombe la AFCON 2023. Lakini ikiwa zimebaki siku mbili tu mashindano kuanza, mchezaji huyo alidaiwa kupata majeraha ya goti ambayo yalihitaji afanyiwe upasuaji na angekaa nje kwa zaidi ya wiki tatu, hivyo akapewa ruhusa ya kuondoka kambini. Badala ya kufanyiwa upasuaji kama ilivyotarajiwakatika hali isiyo ya kawaida mchezaji huyo alionekana akicheza kwenye mchezo huo nchini Hispania. Kocha wa Nigeria Jose Peseiro alipoulizwa kuhusiana na sakata hilo alisema ameshangazwa kwa sababu alipokea ripoti kutoka madaktari wa timu ambao walimwambia kwamba staa huyo hatoweza kuru...

Maajabu ya kikongwe wa miaka 72 nchini Moroco

  Leo nimependa kukuletea habari ya kushangaza na yenye kusisimua ya mzee mmoja   wa miaka sabini na mbili (72) anayejihusisha na uuzaji wa vitabu jijini Rabat nchiI Morocco. Huyu mzee anafahamika kwa jina la Mohammed Aziz, licha ya kuwa muuzaji maarufu wa vitabu katika jiji hilo mzee Mohammed amekuwa akishangaza wengi na kuwaacha midomo wazi kwa uwezo wake wa kutumia masaa sita (6) hadi nane (8) kwa siku kusoma vitabu. Akiwa amesoma zaidi ya vitabu 5,000 vilivyo katika lugha ya Kifaransa, Kiarabu na Kiingereza anabaki kuwa muuzaji   mkongwe zaidi ikiwa hadi sasa ana miaka zaidi ya Arobaini na tano (45) katika biashara hiyo akiwa katika eneo hilohilo bila kuhama hata mara moja. Mzee Mohammed anazidi kuwashangaza wengi kwani mzee huyu huacha zaidi ya vitabu 43 nje ambako vingeweza kuibwa lakini hakuna hata kitabu kimoja kinachopotea au kuibiwa. Vyanzo vya habari maarufu nchini humo vilifanya mahojiano nae na kumuuliza kwanini amekua akijiamini kuacha baadh ya vitab...