Leo nimependa kukuletea habari ya kushangaza na yenye kusisimua ya mzee mmoja wa miaka sabini na mbili (72) anayejihusisha na uuzaji wa vitabu jijini Rabat nchiI Morocco.
Huyu mzee anafahamika kwa jina la Mohammed Aziz, licha ya kuwa muuzaji maarufu wa vitabu katika jiji hilo mzee Mohammed amekuwa akishangaza wengi na kuwaacha midomo wazi kwa uwezo wake wa kutumia masaa sita (6) hadi nane (8) kwa siku kusoma vitabu.
Akiwa amesoma zaidi ya vitabu 5,000 vilivyo katika lugha ya Kifaransa, Kiarabu na Kiingereza anabaki kuwa muuzaji mkongwe zaidi ikiwa hadi sasa ana miaka zaidi ya Arobaini na tano (45) katika biashara hiyo akiwa katika eneo hilohilo bila kuhama hata mara moja.
Mzee Mohammed anazidi kuwashangaza wengi kwani mzee huyu huacha zaidi ya vitabu 43 nje ambako vingeweza kuibwa lakini hakuna hata kitabu kimoja kinachopotea au kuibiwa.
Vyanzo vya habari maarufu nchini humo vilifanya mahojiano nae na kumuuliza kwanini amekua akijiamini kuacha baadh ya vitabu vyake nje ya duka bila kuogopa wezi , alijibu kwa kusema “Wasioweza kusoma hawawezi kuiba vitabu, na wale wanaojua kusoma siyo wezi.”
Mzee Mohammed anatufundisha kitu kimoja muhimu sana juu ya kupata elimu na maarifa kwa kupitia njia ya usomaji wa vitabu. Alimalizia kwa kusema kuwa katika vitabu kuna maarifa makubwa sana lakini watu wengi haswa waafrika wamekosa tamaduni za kujisomea na badala yake kupoteza muda katika kushiriki mambo mengine ambayo hayana tija yoyote katika maisha yao.

Kibongobongo hata wasomi wenyewe wangemuibia mapema tu
ReplyDelete