1. NI SHERIA GANI INAYOSIMAMIA MIKATABA AJIRA TANZANIA?
Kwa ujumla Sheria ya Mikataba inasimamia aina zote za mikataba Tanzania. Lakini kwa mikataba mahususi kuna sheria mahususi inayosimamia mikataba hiyo. Kwa mfano Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi inaelezea mikataba ya ajira. Kwa maana hiyo ni sawa kusema Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2004 pamoja na Sheria ya Mikataba zote zinasimamia mikataba ya ajira.
KUNA AINA NGAPI ZA MIKATABA?
Kuna aina kuu tatu (3) za mikataba ambazo unaweza kuajiriwa nayo, nazo ni:
• Mkataba kwa kipindi cha muda usiotajwa: Kama jina linavyojieleza, kwa aina hii ya mkataba kipindi cha ajira hakiainishwi. Mara nyingine huitwa mkataba wa kudumu.
• Mkataba kwa kipindi cha muda kilichotajwa: Hii ni aina ya mkataba ambao umetaja kipindi cha muda. Chini ya mkataba huu kama kipindi kilichotajwa kikimalizika basi mkataba utakua umefikia mwisho. Mkataba wa kipindi cha muda uliotajwa unaweza kua kwa kipindi cha mwezi, miezi mitatu, mwaka mmoja, miaka miwili nakadhalika.
• Mkataba wa kazi maalumu: Hii ni aina ya mkataba ambapo mtu huajiriwa kufanya kazi maalumu. Pindi kazi inapoisha na mkataba hufikia mwisho. Kwa mfano, mtu anaweza kuajiriwa kushusha kreti za soda kutoka kwenye gari na pindi kazi ile inapoisha na mkataba hufikia mwisho.
2. MKATABA WAKO LAZIMA UONYESHE MAMBO YAFUATAYO:
• Jina, umri, anuani ya kudumu na jinsia ya mfanyakazi
• Mahali alipoajiriwa
• Kazi yake
• Tarehe ya kuanza
• Muundo na muda wa mkataba
• Kituo cha kazi
• Saa za kazi
• Ujira(mshahara), njia za ukukotoaji wake na taarifa za mafao mengine au malipo ya vitu; na
• Kitu kingine kilichotajwa
Kama maelezo yaliyoelezwa hapo juu yamekwisha elezwa katika mkataba ulioandikwa na kupewa mfanyakazi basi mwajiri hana haja ya kumpa mfanyakazi taarifa ya maelezo ya maandishi. Ni jukumu la mwajiri kuhakikisha kwamba maelezo yote au vipengele vya mkataba vinaelezwa katika hali inayoeleweka na mfanyakazi. Ni muhimu kuweka mkataba katika lugha inayoeleweka kirahisi na mfanyakazi, iwe Kiingereza ama Kiswahili.
Kama una swali usisite kuwasiliana nami kwenye sehemu ya comments.
.png)
Comments
Post a Comment