Dakika ya 73 ya mchezo wa kombe la mfalme maarufu kwa jina la Copa Del Rey nchini Hispania kati ya Osasuna na Real Sociedad January 17, Kocha wa Real sociedad alimnyanyua Umar Sadiq kutoka benchi na kumuingiza ili kuchukua nafasi ya Andre Silva.
Tukio hilo la staa huyo wa Nigeria liliwashangaza wengi uwanjani kwani mchezaji huyo alikua kwenye kikosi cha timu ya taifa kule Abidjan nchini Ivory Coast akijiandaa kucheza kombe la AFCON 2023. Lakini ikiwa zimebaki siku mbili tu mashindano kuanza, mchezaji huyo alidaiwa kupata majeraha ya goti ambayo yalihitaji afanyiwe upasuaji na angekaa nje kwa zaidi ya wiki tatu, hivyo akapewa ruhusa ya kuondoka kambini.
Badala ya kufanyiwa upasuaji kama ilivyotarajiwakatika hali isiyo ya kawaida mchezaji huyo alionekana akicheza kwenye mchezo huo nchini Hispania.
Kocha wa Nigeria Jose Peseiro alipoulizwa kuhusiana na sakata hilo alisema ameshangazwa kwa sababu alipokea ripoti kutoka madaktari wa timu ambao walimwambia kwamba staa huyo hatoweza kurudi kwenye hali yake na alihitaji angalau siku 14 ili kuwa fiti.

Comments
Post a Comment