Kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, raia ana haki zifuatazo anapokamatwa na askari polisi:
1. Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwake.
Mwulize jina lake
Mwulize namba yake ya uaskari
2. Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka au kukamatwa.
3. Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa au sehemu anakofanyia kazi kwamba amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
4. Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi au Taasisi ya kuzuia rushwa.
5. Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana Iwapo kituo cha polisi au Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
6. Raia ana haki ya kuwaeleza polisi au Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
7. Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi au Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
8. Raia ana haki ya kuyasoma maelezo kabla ya kutia sahihi yake.
9. Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa au kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
10. Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
11. Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
12. Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi KABLA ya kupekuliwa yeye mwenyewe
13. Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa:
(a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani,
(b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au
(c) jirani wa mtu anayetuhumiwa,
14. Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale.

Comments
Post a Comment