Skip to main content

Funzo kuhusu vijana na maisha.

 

VIJANA WENGI UKIWATIZAMA UTAWAONA KAMA WANA FURAHA LAKINI NYUMA YA PAZIA WANATESEKA SANA NA UMASIKINI.

Ni kawaida sana kwa siku hizi kukuta binti wa kike mrembo au kijana wa kiume mtanashati, msomiamemaliza chuo kikuu anamiliki simu kali yaani nzuri sana na yenye gharama kubwa. Wapo pia wanaopendeza kwa nguo nzuri na manukato ya bei kubwa kila utakapowaona huenda hata ukatamani kuwa kama wao.

Lakini ukifuatilia nyuma ya pazia hawa vijana wanateseka sana na ugumu wa maisha huku wimbi la ukosefu wa kazi na kipato likizidi kuwatawala. Maumivu wanayopitia ni makubwa mno kuliko unavyoweza kuwaona kwenye sura zao za nje (ambazo ni feki)

Kwa isivyo bahati hata wale vijana waliopo vyuo vikuu wanapitia changamoto hii na wala hawajashtuka mapema. Wengi wanakuja kushtuka baadae sana ambapo muda unakua umeshawatupa mkono, Too late!!! Wanaishia kutembeza bahasha za maombi ya kazi kwenye maofisi wanaishia kuonekana kama omba omba tu.

Kijana kama unajitambua jitahidi upate maarifa ya biashara uanze kujenga biashara yako, haya mambo ya kusubiria kuajiriwa ni utumwa, tena ni utumwa uliopitiliza.

Wewe kama kijana unajitambua na unatamani kuondokana na hali hii ya maisha feki ya kuonekana uko vizuri kimaisha kumbe shida zimekujaa usisite kuwasiliana nami, nitakufundisha namna ya kuweza kujipatia kipato na kujikomboa kutoka umaskini. Endelea kufuatilia Mopao media kwa elimu zaidi juu ya maisha.

Comments

Popular posts from this blog

Nyumba ya P.Diddy yavamiwa na maafisa usalama

  Nyumba ya mfanyabiashara na mwanamuziki maarufu nchini Marekani P.Diddy ambaye sasa hivi anajiita DIDDY imevamiwa na maafisa wa usalama wa nchini Marekani kwa ajili ya upekuzi na uchunguzi. Maafisa wa usalama hao walivamia nyumba ya Diddy na kuwafunga pingu watoto wake wawili wanaofahamika kwa majina ya King na Justin wakati huo huo baba yao ikiwa hajulikani alipo. Inasemekana mara ya mwisho ndege ya Diddy ilikuwa ikionekana angani kuelekea visiwa vya Carribean. Diddy anashutumiwa kujihusisha na biashara haramu za ngono na biashara ya binadamu na hii ndiyo sababu uvamizi huo umefanyika katika nyumba yake. 

Kwanini Mungu hajibu maombi yetu?

  Wakati mwingine tumekuwa tukiomba sana kwa Mungu lakini hatupokei majibu. Leo tutajifunza mambo 10 yanayosababisha maombi yetu kutojibiwa. 1) DHAMBI. Baada ya mwanadamu kuasi pale Eden dhambi iliingia ulimwenguni na kila aliyezaliwa alikua na dhambi. Lakini hii haikumaanisha kwamba tukiomba Mungu hatusikii, bali ilimaanisha ili Mungu atusikie,t ulipaswa kwanza kutubia makosa na dhambi zetu ndipo tumueleze Mungu matatizo yetu. Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo. Yohana 9:31   lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. Hivyo basi kabla hujampelekea Mungu matatizo/shida yako hakikisha mahusiano yenu yako vizuri.  2) KUKOSA IMANI. Nadhani hii ni miongoni mwa sababu kubwa  inayofanya watu wasipokee majibu ya maombi yao. Wa e brania 11:6  Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana m...

Imamu shoga auliwa na wasiojulikana

  M uhsin Hendricks, mtu mashuhuri aliyejulikana kama imamu wa kwanza duniani aliyejitangaza hadharani kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja, ameuwa kwa risasi nchini Afrika Kusini. Kiongozi huyo wa kidini mwenye umri wa miaka 57 alikuwa anaongoza msikiti mmoja katika jijini la Cape Town uliolenga kuwa mahali salama na kimbilio kwa waumini wa kiislamu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja na wale waliotengwa na jamii. Alipigwa risasi Jumamosi asubuhi baada ya gari alilokuwa akisafiria karibu na jiji la kusini la Gqeberha kushambuliwa. "Washukiwa wawili wasiojulikana wakiwa wamefunika nyuso zao walitoka kwenye gari ingine na kuanza kulimiminia risasi nyingi gari hilo," polisi walisema katika taarifa yao. Habari za kifo cha Hendricks zimeleta mshtuko mkubwa katika jamii ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja (LGBTQ+ ) na kwingineko, huku kukitolewa salamu nyingi za rambirambi kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Julia Ehrt, mkurugenzi mtendaji wa shirika la Internati...